mgombea ubunge kinondoni kwa tiketi ya cuf Rajabu juma ajigamba kwa maneno mazito
Mgombea ubunge jimbo la kinondoni kwa tiketi ya cuf Rajabu juma ajigamba kwa maneno mazito.
Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CUF Rajabu Juma amejigamba kwamba yeye ni mzawa halisi wa Kinondoni kwa sababu amezaliwa Mwananyamala Hospitalini.
Amesema kwamba kwa sababu yeye ni mzawa wa eneo hilo anazijua fika changamoto za jimbo lake hivyo anawaomba wapiga kura wasiache kumchagua.
“Mimi ni mzawa wa hapa nimezaliwa hapo Mwananyamala Hospitali naombeni kura zenu msiache kunichagua jamani nitahakikisha nazitatua changamoto za hapa’’ amesema na kuongeza
‘’Leo nimeja hapa kuzungumza na nyinyi kujua shida zenu, nipeni kura tarehe 17 niwe mbunge wenu’’.
‘’Leo hii uchaguzi unarudiwa na kutumia pesa nyingi za maendeleo kwa sababu ya mbunge aliyekuwepo , leo anarudi tena kuomba kura, huyu hafai’’ amesema

Comments
Post a Comment